Mmiliki wa Timu ya TP Mazembe Ahukumiwa Kifungo Jela Miaka Mitatu


Mgombea urais wa upinzani nchini Jamhuri ya Demokrasi ya Congo Moise Katumbi, amehukumiwa kifungo cha miaka 3 jela kwa kununua nyumba kinyume cha sheria kwenye mji ulio mashariki mwa nchi wa Lubumbashi.

Pia alipigwa faini ya dola milioni 6.

Katumbi hakuwa mahakamani wakati wa kutolewa kwa hukumu hiyo, baada ya kusafiri kwenda afrika kusini kupata matibabu siku moja baada ya serikali kutangaza waranti wa kukamatwa kwake kwa mashtaka tofauti.

Analaumiwa kwa kuwaajiri mamluki wa kigeni ili kipanga njama dhidi ya serikali.
Katumbi amekosoa hukumu hiyo, akisema kuwa ni jaribio la kutaka kuchelewesha kampeni yake ya kutaka kumrithi Rais Joseph Kabila mwezi Novemba.
Mmiliki wa Timu ya TP Mazembe Ahukumiwa Kifungo Jela Miaka Mitatu Mmiliki wa Timu ya TP Mazembe Ahukumiwa Kifungo Jela Miaka Mitatu Reviewed by Unknown on 11:31:00 Rating: 5

Hakuna maoni:

Facebook

klin zepp. Inaendeshwa na Blogger.