Hizi Hapa Sababu za Zari Kupungua Mwili Mobetto Atajwa

Hizi Hapa Sababu za Zari Kupungua Mwili Mobetto Atajwa
Mwanamitindo Hamisa Mobeto amedaiwa kuwa sehemu ya kupungua mwili kwa mwanadada mjasiriamali maarufu, Zarina Hassan ‘Zari The Boss Lady’.

Kwa mujibu wa chanzo makini, tangu Mobeto aanze kuibua mjadala mtandaoni kuhusiana na mtoto wake kudaiwa kuwa ni wa bwana wa Zari, mjasiriamali huyo amejikuta akipungua mwili kutokana na mawazo aliyonayo.

“Zari kapungua mwili kweli jamani. Mobeto amemponza. Amemsababishia watu wamtukane sana Zari kiasi ambacho amekosa amani kabisa. Masikini mtoto wa watu kakonda kweli sasa hivi.

“Ukitazama picha za Zari sasa hivi si Zari yule aliyetoka kujifungua. Tena kwa kawaida tunajua mtu ukitoka kujifungua unanenepa lakini kwa Zari mambo yamekuwa tofauti. Ngoja niwatumie picha yake ya sasa muone,” kilisema chanzo.

Hata hivyo mwanahabari wetu aliingia kwenye ukurasa wa Instagram wa Zari na kujionea jinsi alivyopungua baada ya kuona picha zake mpya na kulinganisha na picha zake za zamani.
Licha ya yeye mwenyewe kutozungumzia suala hilo lakini mashabiki wake walisema amefanya vizuri kujipunguza unene kwani sasa ametokelezea tofauti na zaman
Hizi Hapa Sababu za Zari Kupungua Mwili Mobetto Atajwa Hizi Hapa Sababu za Zari Kupungua Mwili Mobetto Atajwa Reviewed by Unknown on 22:37:00 Rating: 5

Hakuna maoni:

Facebook

klin zepp. Inaendeshwa na Blogger.