Rais wa TFF anayemaliza muda wake Jamal Malinzi amewatumia salamu viongozi wa TFF na kuwatakia uchaguzi mwema unaotarajiwa kufanyika mwezi Agosti mwaka huu.
Aidha, Malinzi katika salamu hizo, ameishukuru Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Dk. John Pombe Joseph Magufuli, wadhamini mbalimbali, washirika na wadau wa soka kwa ushirikiano walioutoa katika kipindi chote cha uongozi wake.
Salamu hizo ambazo zimetolewa kupitiwa kwa mawakili wake zilieleza kuwa anaamini kwamba TFF watafanya uchaguzi vizuri na viongozi watakaopatikana wataweza kuendeleza programu muhimu.
Malinzi alilazimika kujiondoa kwenye uongozi wa TFF na kushindwa kutetea nafasi yake baada ya kuwekwa rumande tangu Juni 29 kwa tuhuma za ubadhirifu na matumizi mabaya ya madaraka.
Malinzi, Katibu wake, Selestine Mwesigwa pamoja na Mhasibu wa TFF, Nsiande Isawafo Mwanga walipelekwa rumande Juni 29 baada ya kusomewa mashitaka 28 ya kughushi na kutakatisha fedha kupitia akaunti ya TFF iliyopo katika banki ya Stanbic, Dar es Salaam
Muimbaji Peter Msechu alijikuta matatizoni wiki iliyopita baada ya kutoa kauli ya mzaha kwamba yeye ni mtu anayefumaniwa kila siku mtaani kwake.
Msechu amedai muda mchache baada ya kauli hiyo kusambaa mke wake alianza kupigiwa simu na watu mbalimbali kitu ambacho kilimfanya achanganyikiwe.
Kauli hiyo aliitoa Msechu baada ya kuulizwa swali na kituo kimoja cha redio kwamba wasichana wengi hawapendi kutoka kimapenzi na wanaume wenye vitambi ndipo muimbaji huyo akajibu mbona yeye mtaani kwake wasichana wengi wanamgombania huku akidhihaki tena ameshikwa ugoni mara kadhaa.
Akiongea Jumatano hii katika kipindi cha Yaliyomoyamo cha Redio One Stereo, Msechu amedai kauli hiyo aliitoa kwa mzaha na baadhi ya watu walishindwa kuielewa.
Katika hatua nyingine muimbaji huyo ambaye anafanya vizuri na wimbo ‘Yakawa’ amedai muziki kwa sasa unawafanya wasanii kubadilisha aina ya muziki waliokuwa wanafanya awali na kuingia kwenye muziki wa kutegemea kiki.
Msechu amedai muda mchache baada ya kauli hiyo kusambaa mke wake alianza kupigiwa simu na watu mbalimbali kitu ambacho kilimfanya achanganyikiwe.
Kauli hiyo aliitoa Msechu baada ya kuulizwa swali na kituo kimoja cha redio kwamba wasichana wengi hawapendi kutoka kimapenzi na wanaume wenye vitambi ndipo muimbaji huyo akajibu mbona yeye mtaani kwake wasichana wengi wanamgombania huku akidhihaki tena ameshikwa ugoni mara kadhaa.
Akiongea Jumatano hii katika kipindi cha Yaliyomoyamo cha Redio One Stereo, Msechu amedai kauli hiyo aliitoa kwa mzaha na baadhi ya watu walishindwa kuielewa.
“Yaani baada ya ile kauli kusambaa hawakunitafuta mimi wala media, wakatafuta mzazi wangu, nilikwambia mwanao mwambie aache muziki sasa angalia anafumaniwa kila siku. Mke wangu akajazwa maneno ametoka ofisini amedata,” alisema Msechu.
Katika hatua nyingine muimbaji huyo ambaye anafanya vizuri na wimbo ‘Yakawa’ amedai muziki kwa sasa unawafanya wasanii kubadilisha aina ya muziki waliokuwa wanafanya awali na kuingia kwenye muziki wa kutegemea kiki.