Jumanne, 19 Julai 2016

Diamond na Mama Mtoto Wake Zari Hassan Wathibitisha Tetesi za Kuwa Wamenunua Nyumba ya Kifahari South Africa


Diamond na Zari wathibitisha uwepo wa Jumba kubwa la kifahari walilonunua South Africa kwaajili ya mtoto wao Tiffah! !! Hakika hapa wametisha mbayaa...unaambiwa hilo Jumba ni shidaaaa...
#ubuyuuuuu

Zari Hassan Awafungukia Wote Wanadai Kuwa Yeye ni Gold Digger Kwa Diamond

Kuna Baadhi ya watu huko mitandaoni wanalalamika kuwa Baby Mama wa Diamond Zari Hassan ni Gold Digger, Kuwa yupo kimaslahi zaidi kwa Diamond na anamchuna ipasavyo...
Baby Mama huyo maneno yamemkuna na kuwafungukia kama ifuatavyo:

'When people call you a gold digger show them how you dig, too much money out there for all of us. Why hate? Stop BITCHCRAFTY it's the 21st century'


Akaendelea Hivi:

'Say YES to this type of gold digging or digging gold. And if your man happens to spoil you its because he can afford it and your his ๐Ÿ‘‘ueen you deserve it..... yes am a GOLD DIGGER ๐Ÿ˜Š coz I earn every that comes my way. Now let's all go and dig some gold

Mlinzi Adaiwa Kujinyonga kwa Kuambukizwa VVU

Mlinzi wa  Kampuni ya  Ulinzi ya Imara , Samwel Alcado (39) amekutwa akiwa amejinyonga ndani ya chumba chake kutokana na kile kinachodaiwa ni kugundulika kuwa ana virusi vya Ukimwi (VVU).
Mlinzi huyo ambaye ni mkazi wa mtaa wa Mji wa Zamani Manispaa ya Mpanda amejinyonga kwa kutumia shati lake.
Mwenyekiti wa mtaa huo, Margret John amesema tukio hilo  limetokea  leo  majira  saa kumi na moja alfajiri ndani ya   chumba alichokuwa  akiishi   Alcado.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi, Damas Nyanda amethibitisha kutokea kwa kifo hicho akisema uchunguzi zaidi unaendelea kufanyika ili kubaini ukweli halisi wa tukio hilo.

TAMKO LA WIZARA KUHUSU MATUMIZI NA USAMBAZAJI WA VILAINISHI KWA AJILI YA UDHIBITI WA MAAMBUKIZI YA UKIMWI

logoWizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imekuwa ikitekeleza afua mbalimbali za mapambano dhidi ya maambukizi ya VVU nchini ambazo zimepelekea kupungua kwa viwango vya maambukizi ya VVU kitaifa kutoka wastani wa asilimia 7 mwaka 2007-2008 hadi kufikia asilimia 5.1 mwaka 2011-2012. Mafanikio haya yamefikiwa kutokana na ushirikiano wa karibu kati ya Wizara na wadau mbalimbali wa maendeleo pamoja na wale wa utekelezaji wa moja kwa moja wanaofanya kazi na mikoa yote Tanzania bara. Aidha kumekuwa na uitikiaji mzuri kutoka kwa wananchi katika utekelezaji wa afua hizo.Sambamba na mafanikio haya, tafiti mbalimbali hapa nchini zimethibitisha kuwepo kwa kiwango cha juu cha maambukizi ya VVU miongoni mwa makundi maalum yaliyo katika hatari zaidi ya maambukizi kuliko kiwango kilichopo miongoni mwa jamii ya kawaida. Makundi haya ni pamoja na Wanawake wanaofanya biashara ya ngono ambayo maambukizi ya VVU ni asilimia 26, Watu wanaojidunga sindano za madawa ya kulevya (asilimia 36) na Wanaume wanaoshiriki ngono baina yao (asilimia 25). Aidha, makundi haya yamekuwa na muingiliano wa karibu sana na wana jamii ya kawaida, na hivyo kupelekea hatari ya kutofanya vizuri katika udhibiti wa maambukizi ya VVU nchini.

Hali hii ilisababisha kuwepo na umuhimu wa kuongeza nguvu katika afua mbalimbali za kukabiliana na ongezeko la maambukizi ya VVU miongoni mwa makundi haya, pamoja na jamii ya kawaida ili kudhibiti VVU. Kwa mantiki hiyo, Wizara kwa kushirikiana na wadau mbali mbali walikubaliana mikakati mahsusi ya kutoa huduma bora na rafiki kwa watu wa makundi maalum kwa kuzingatia sheria, taratibu, mila na desturi za taifa letu.
Pamoja na nia njema na jitihada za pamoja baina ya Wizara na wadau katika mapambano dhidi ya UKIMWI, imebainika kwamba baadhi ya wadau wanaotekeleza shughuli za makundi maalum wamekuwa wakikiuka taratibu za kiutendaji hasa suala la kuihusisha Wizara na Mikoa husika wanakofanyia kazi kuhusu uanzishwaji na/au utekelezaji wa baadhi ya shughuli wanazozifanya. Aidha pia katika baadhi ya maeneo, wadau hao wamekuwa wakitekeleza shughuli ambazo ziko kinyume na makubaliano waliyoingia na Wizara ya Afya.
Miongoni mwa shughuli zinazokinzana na mila na desturi zetu ni pamoja na usambazaji wa vilainishi. Ni kweli kuwa Wizara imezuia usambazaji wa vilainishi na tayari tumewasiliana na wadau hao ambao wameahidi yafuatayo:
  • Kukusanya vilainishi vilivyokuwa vimesambazwa na kuhakikisha kuwa vinateketezwa
  • Imekubalika pia kuwa wadau kwa kushirikiana na Wizara watakaa pamoja na kuangalia endapo pana fedha ambazo zingetumika kununua vilainishi, basi fedha hizo ziweze kupangiwa matumizi stahiki kulingana na vipaumbele vya Wizara na taifa kwa ujumla.
Wizara inawapongeza na kuwashukuru wadau wote kwa jitihada za dhati zinazoendelea kutekelezwa na katika kusimamia kikamilifu miongozo inayotolewa na Wizara yenye lengo la udhibiti wa ugonjwa wa UKIMWI.
Imetolewa na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto
19 Julai 2016

WANAFUNZI 7800 WALIOFUKUZWA UDOM, NI 382 TU NDIO WENYE SIFA


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako akizungumza na waandishi habari juu ya hatua ya serikali waliochukua kwa wanafunzi waliondolewa katika chuo kikuu cha Dodoma leo ofisini kwake jijini Dar es Salaam, Kulia ni Naibu Katibu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dk. Leonard Akwilapo, Kulia ni Kamishina wa Elimu wa Wizara hiyo, Eustella Balamsesa.
Serikali imetangaza orodha ya wanafunzi ambao watarejea kuendelea na masomo katika Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) baada ya uchambuzi kumalizika na kupatikana idadi ya wanafunzi ambao wana sifa za kuendelea na masomo.Akizungumza na waandishi wa habari, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Joyce Ndalichako alisema kuwa kwa kipindi chote walikuwa wakifanya uchambuzi ili kuona ni wanafunzi gani walikuwa na sifa za kusoma kozi hiyo maalum ambayo ilianzishwa kutokana na tatizo la walimu wa Sayansi.
Alisema kuwa programu hiyo ilikuwa inahitaji walimu ambao watakwenda kufundisha shule za sekondari lakini kulikuwa na wanafunzi 1,210 ambao walikuwa wanachukua stashahada ya ualimu wa shule za msingi ambao ni kinyume na malengo na 6,595 wakichukua stashahada ya kufundisha shule za sekondari.

“Baada ya hatua ya kuwaondoa wanafunzi chuoni kuchukuliwa, serikali ilifanya uchambuzi wa wanafunzi hao kwa lengo la kujiridhisha na sifa zao. Sifa zilizotakiwa ni ufaulu wa daraja la 1 hadi daraja la 3 na krediti mbili au zaidi katika masomo ya Sayansi na Hisabati,

“Lakini baada ya uchambuzi kufanyika kati ya wanafunzi wanaosomea ualimu wa sekondari 6,595 ni wanafunzi 382 pekee ndiyo wana sifa za kuendelea na masomo yao, 134 ni mwaka wa kwanza na 248 ni mwaka wa pili,” alisema Prof. Ndalichako.

Aidha alisema kuwa wengine 4,586 wa mwaka wa kwanza wa programu maalum wa stashahada ya ualimu wa sekondari waliokidhi vigezo vya ufaulu watahamishiwa katika vyuo vya ualimu vya serikali ambavyo ni Morogoro, Butimba, Mpwapwa, Songea na Tukuyu kuendelea na masomo na wanafunzi 1,337 wa mwaka wa pili watahamishiwa vyuo vya Korogwe na Kasulu ili kumalizia masomo yao.

Pia alisema kuwa serikali itaendelea kuwapatia mikopo wanafunzi watakaoendelea kusoma UDOM na watarejea chuoni mwezi Oktoba mwaka huu, huku wale wa vyuo vya ualimu watakuwa wakilipiwa ada ya 600,000 kwa mwaka ambayo ndiyo ada ya vyuo hivyo na wataripoti chuoni mwezi Septemba.

Kwa upande wa wanafunzi wa kufundisha elimu ya shule ya msingi, Prof. Ndalichako alisema wanafunzi 29 wa mwaka wa pili ambao wana cheti cha daraja A la ualimu watahamishiwa Chuo cha Ualimu Kasulu ili wamalize masomo yao ila tu kwa gharama zao huku wengine 1,181 akiwataka waombe nafasi katika vyuo vingine katika masomo ambayo wana sifa zinazolingana nao.

Aidha katika hatua nyingine, Prof. Ndalichako alisema kuwa migomo iliyokuwa ikitokea chuoni UDOM kwa walimu kugoma kuwafundisha wanafunzi hao yawezekana ilikuwa ikichangiwa na wanafunzi hao kwani uwezo wa chuo cha UDOM ilikuwa ni kupokea wanafunzi 1,180 lakini wakapokea wanafunzi 7,805.

“Walimu kwao mzigo ulikuwa ni mzito wewe utafanya nini?, kwahiyo tukubali kuwa wingi wa wanafunzi ulichangia kutokea mgomo sababu walimu wameajiriwa kufundisha na wengine wa digrii sasa kupokea wanafunzi 7,805 na ilitakiwa 1,180 walikuwa wengi,” alisema Prof. Ndalichako.

Uhusiano Uliopo Kati ya Punyeto na Upungufu wa Nguvu za Kiume Kwa Mwanaume......


 UKOSEFU  ama  upungufu  wa  nguvu  za  kiume, ni  tatizo  linalo  wakabili  mamilioni  ya  wanaume  duniani.

 Zipo  sababu  nyingi  zinazo  sababisha  tatizo  la  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume, Miongoni  mwa  sababu  hizo  ni  pamoja  na  maradhi  kisukari, presha,shinikizo  la  damu, moyo, figo, matatizo  kwenye  mishipa  ya  ubongo  &  mishipa  ya  uti  wa mgongo, matatizo  kwenye  mishipa itumikayo  kusafrisha damu  mwilini, maradhi  ya  ngiri,  pamoja  na   upigaji  punyeto  kwa  muda  mrefu.

Katika  makala  yetu  ya  leo, tutaangalia  namna   suala  la  upigaji  punyeto linavyo  athiri  nguvu  za  kiume.

Ukisoma  vizuri  kuhusu  mfumo  wa  nguvu  za  kiume, utagundua  kuwa   Suala  la  nguvu  za  kiume  ni  suala  la  kimfumo.  Ili  mwanaume  awe na nguvu  za  kiume, aendelee  kuwa  na  nguvu  za  kiume na  azilinde  nguvu  zake za  kiume, ni  lazima  ogani  zote zinazo  husika  na  mfumo  wa  nguvu  za  kiume  ziwe  na  afya  njema  na  ziwe  na  ushirikiano   thabiti  na  wenye  afya.
Vile  vile , utagundua  kuwa , mambo  makuu  muhimu  katika   mfumo  wa  nguvu  za  kiume  ni  kama  ifuatavyo:


  1. Mishipa  imara  ya  ubongo  na  yenye  afya  njema
  2. Mishipa  imara  ya  uti  wa  mgongo  (  spinal  cords )
  3. Mishipa  imara  itumikayo  kusafirisha  damu  mwilini  (  Blood Vessels )
  4. Mfumo  imara  wa  usafirishaji  damu  mwilini
  5. Mishipa  ya  uume  iliyo  imara  na  yenye  afya  njema
  6. Uhusiano  imara  na  wenye  afya  kati  ya  mishipa  ya  fahamu  iliyopo  katika  ubongo, mishipa  ya  kwenye  uti  wa  mgongo  pamoja  na  misuli & mishipa  ya  kwenye  uume.


Hivyo  basi, ili  mwanaume  aweze  kuwa  na  nguvu  imara  za  kiume, na  aendelee  kuwa  na  nguvu  hizo ni  lazima  mambo  yote  muhimu  katika  mfumo  wa  nguvu za  kiume  yawe  imara  pasi na  hitilafu  yoyote.

Hitilafu  yoyote  katika  mambo  hayo, itasababisha  ukosefu na/ama  upungufu wa  nguvu  za  kiume  kwa  mwanaume  huyo.  Pale inapotokea    hitilafu  ama  mapungufu  katika  ogani  zaidi  ya  moja  kati  ya  zilizo  tajwa hapo  juu, basi  tatizo  kwa  muhusika  huwa  kubwa  mara  dufu.

JINSI  PUNYETO  INAVYO  SABABISHA  TATIZO  LA  UKOSEFU &  UPUNGUFU  WA  NGUVU  ZA  KIUME.
Mwanaume   anapopatwa na  wazo  la  kufanya  tendo  la  ndoa, ubongo  hutoa  ishara  kwenye  mishipa  ya  uti  wa  mgongo  ambayo  nayo  husafirisha  taarifa  hadi  kwenye  mishipa &  misuli  ya  uume. Mishipa  ya  uume inapopokea  taarifa  hiyo, hutanuka.

Na  mishipa  ya  uume  inapotanuka, hufanya  mambo  mawili  muhimu  sana :

  • Husababisha  mishipa  ya  ateri  kupanuka  na  hivyo  kuruhusu  damu  kuingia kwa  kasi  sana   ndani  ya  mishipa  ya  uume  na  hivyo  kuufanya  uume  usimame  na  kuwa  imara  bara bara.
  • Huibinya na  kuiziba  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kuzuia  kunyonya  ama  kufyonza  damu  iliyo  ingia  ndani  ya  mishipa ya  uume.  (  KAZI  KUBWA  YA  MISHIPA  YA  VENA  ILIYO  KARIBU NA  MISHIPA  YA  UUME  NI KUHAKIKISHA  HAKUNA  DAMU NDANI YA  MISHIPA  YA  UUME. HIVYO  BASI  DAMU  INAPOINGIA  NDANI YA  MISHIPA  YA  UUME, MISHIPA  YA  VENA  HU “SENSE” JAMBO  HILO  KWA  HARAKA  NA HIVYO  KUIFYONZA  DAMU  HIYO  KUTOKA KWENYE MISHIPA  YA UUME  YA  KUITOA  NJE YA MISHIPA  YA  UUME.  NA  DAMU INAPOKOSEKANA  NDANI  YA  MISHIPA  YA  UUME, HUUFANYA  UUME  KUSINYAA  NA  KULEGEA)


Mtu  anayepiga  punyeto  husababisha  mambo  yafuatayo  katika  mwili  wake :

  • Huuwa  nguvu  ya  mishipa  & misuli ya  uume ambayo  ndio  inayo husika  na  kusimama  kwa  uume
  • Mishipa  ya   uume  inapo  sinyaa  na  kukosa  nguvu  yake  ya  asili, husababisha  mambo  yafuatayo :


  1. Huondoa  uwezo  wa  mishipa  &  misuli  ya  uume  kutanuka, na  hii  ndio  sababu  inayo  wafanya  waathirika  wa  punyeto  kutumia  nguvu  nyingi  sana  katika  kuufanya  uume  usimame.
  2. Huondoa  uwezo  wa  mishipa &  misuli  ya  uume  kuibana  na  kuiziba  mishipa  ya  vena, na  hii ndio  sababu  inayo  fanya  waathirika  wa  punyeto  kufika  kileleni  haraka  sana, kwani damu  inayo  ingia  kwenye misuli  ya  uume   hufyonzwa  ndani ya  muda  mfupi sana.  Hii  hutokea  kwa  sababu  mishipa na  misuli  ya  uume inakuwa  imelegea,na  mishipa  ya  vena inakuwa  imepwaya, hivyo  msuguano wowote ule  hufanya  mishipa  ya  vena  kufunguka  na  kufyonza  damu  kutoka  kwenye mishipa  ya  uume  na hivyo  kuufanya  uume  kusinyaa  ndani ya dakika ama sekunde  chache sana.



  • Vile  vile  punyeto  hufanya  uume  kusinyaa na  kurudi ndani  na  kuufanya  uonekane kama  uume  wa  motto mdogo.

Kwa  ufupi  punyeto  husababisha  ukosefu  wa  nguvu  za  kiume  kwa  sababu  kuu  zifuatazo :

  • Kwanza   hudhoofisha  na  kuharibu  mishipa  ya  uume,  ambayo  ndio  hufanya  uume kusimama.
  • Pili  hudhoofisha  utendaji  kazi  wa  mishipa  ya  ateri, ambayo  ndio  hutumika  kama  njia  ya  kusafirisha  damu kupeleka kwenye  misuli  ya  uume  na  ivyo  kuufanya  uume  usimame
  • Tatu, punyeto  hupelekea  kuvuja  kwa  mishipa  ya  vena  na  hivyo  kusababisha  damu  kufyonzwa  kwa  haraka  sana  kila  iingiapo ndani  ya  misuli ya  uume  na  matokeo  yake  ni  uume   kusimama  kwa  muda  mfupi  sana  wakati wa  tendo  la  ndoa
  • Punyeto  huathiri  mtiririko  wa  damu  kwenda  kwenye  mishipa  ya  uume, kwa  sababu  hudhoofisha  misuli &  mishipa  ya  uume  pamoja  na mishipa ya  ateri  ambayo  ndio  hutumika  katika  kusafirisha  damu kwenda  kwenye  uume


DALILI  ZA  MTU  ALIYE  ATHIRIWA  NA  PUNYETO

Dalili  kuu  za  mtu  aliye athiriwa  na  punyeto  ni  kama  ifuatavyo:

  • Uume  kusinyaa  na  kuwa  kama  wa  mtoto
  • Uume kurudi  ndani
  • Uume  kusimama  ukiwa  legelege
  • Kufika  kileleni  haraka  wakati  wa  tendo  la  ndoa.

USHAURI; Jinsi Ya Kuondokana Na Matumizi Mabaya Ya Mtandao Wa Intaneti Na Kutumia Vizuri Muda Wako Kujiongezea Kipato.

Kama kuna mapinduzi ambayo kizazi hiki kinayashuhudia kwa macho basi ni mapinduzi ya kiteknolojia hasa kwenye kompyuta na mtandao wa intaneti. Mapinduzi mengi yaliyotokea huko nyuma hatukuwepo, tumekuwa tunayasikia tu kama mapinduzi ya viwanda.

Uzuri wa kuwa hai wakati wa mapinduzi ni kwamba unakuwa na nafasi kubwa ya kunufaika na mapinduzi hayo kuliko wale wanaokuja baadaye au waliochelewa kuyatumia mapinduzi hayo.

Kwa mfano watu wengi ambao wanashikilia rekodi ya kuwa matajiri sana duniani walitokana na mapinduzi ya viwanda yaliyotokea karne ya 19 ulaya na marekani.

Watu kama John Rockefeller walitumia vizuri mapinduzi ya viwanda kujijengea utajiri mkubwa.

Tukija kwenye zama zetu hizi za mapinduzi ya kiteknolojia, tunaona jinsi ambavyo mtandao wa intaneti umezalisha mabilionea wakubwa duniani.

Watu kama Mark Zuckerberg, mmiliki wa mtandao wa Facebook ni bilionea aliyezalishwa na mapinduzi haya ya kiteknolojia.

Wapo wengi ambao wananufaika sana na mapinduzi haya, swali ni je wewe unanufaikaje na mapinduzi haya? Hili ni swali muhimu tunalopaswa kujiuliza kila siku.

Mtandao wa intaneti umekuja na faida nyingi sana kwetu, kuanzia kuboresha kazi zetu, biashara zetu na hata maisha yetu kwa ujumla. Sasa hivi ni rahisi kutangaza biashara na hata kuwafikia wateja popote walipo duniani. Ni rahisi kuwasiliana na ndugu jamaa na marafiki popote pale walipo.

Lakini kila chenye faida hakikosi hasara, na mtandao wa intaneti umekuwa na hasara nyingi ambazo zimewazuia watu kupata mafanikio makubwa kwenye maisha yao. Mtandao wa intaneti umekuwa na ulevi mkubwa hasa kwa watumiaji ambao unawafanya washindwe kuweka muda kwenye yale mambo ya muhimu kwao.

 Leo kupitia makala hii ya ushauri wa changamoto tutaona jinsi ya kuondokana na ulevi huu ili kuweza kutumia muda wetu vizuri na kufikia malengo yetu.

Kabla hatujaangalia kwa undani hatua za kuchukua, tupate maoni ya msomaji mwenzetu aliyetuandikia kuhusiana na changamoto hii.

Jambo la kwanza; kuwa na utaratibu maalumu wa kutembelea mitandao hii. 
Moja ya kitu kinachofanya matumizi ya mitandao kuwa changamoto ni ukaribu wake na urahisi wa kuitumia. Kwa kuwa mitandao hii ipo kwenye mikono yetu, nikimaanisha simu zetu za mkononi, ni rahisi sana kuingia hasa pale unapopata hata dakika moja.

Urahisi huu unafanya tukiwa na upweke kidogo tu tufungue mitandao. Baadaye tunaingiwa na hofu kamba tusipofungua muda mrefu basi tunapitwa, na hivyo tunajikuta kila baada ya dakika chache tunachungulia tena tuone kipi kipya.

Utafiti uliowahi kufanywa, kuhusiana na simu hizi za kiganjani, unaonesha watu wanazishika simu zao mara nyingi mno, na mara zote ni kwenye mitandao ya kijamii.

Ili kuondokana na ulevi huu, jiwekee utaratibu wa kuingia kwenye mitandao hii ya kijamii kwa muda fulani wa siku. usikubali kila dakika uwe ‘online’, jitengee muda maalumu kila siku au kila baada ya masaa fulani ndiyo uingie kwenye mitandao hii. Muda mwingine uweke kwa ajili ya kazi na zima kabisa data kwenye simu yako.

Unapokuwa kwenye kazi ambayo inahitaji umakini, usikatishe ili kuingia kwenye mitandao, kwani unaporudi kwenye kazi yako unapoteza muda mwingi zaidi.

Jambo la pili; ondoa taarifa za mitandao ya kijamii unazopata kupitia simu yako.
Kwenye simu zetu kuna kitu kinaitwa ‘notification’ hii ni ile taarifa ambayo simu yako inakupa kwamba kuna mtu kakutumia ujumbe, au kapenda picha yako kwenye mtandao.

Taarifa hizi zina nguvu ya kukusukuma uchukue hatua haraka kuona ni ujumbe gani umetumiwa au nani kasema nini kuhusu ulichoweka kwenye mitandao.

Ili kuondokana na hili, futa kabisa kupotea taarifa hizi za kila kinachoendelea kwenye mitandao. Kwa njia hii hutasukumwa kufungua badala yake utafungua pale muda wako uliojipangia unapokuwa umefika.

Na kama unaona huwezi kuondoa notification, ondoa kabisa zile application ambazo ni za mitandao ya kijamii, na badala yake uwe unaingia moja kwa moja kupitia mtandao. Siyo lazima uwe na app zote za kufungua kila aina ya mtandao, kwa sababu kwa kuwa nazo utajikuta umetengeneza utaratibu wa kuzunguka kwenye mitandao hii.

 Kwa mfano unaanza na facebook, unaangalia kisha unaenda instagram, ukimaliza unaenda snapchat, unatoka hapo unaingia wasap, kisha telegram, ukifika huko ni muda unarudi kuangalia tena kama kuna jipya facebook, kisha instagram, na unajikuta unarudia mzunguko mzima hata mara tatu. Ukiondoa zile app ambazo siyo muhimu sana utapunguza kutembelea ile mitandao ambayo siyo muhimu kwako.

Jambo la tatu; nufaika na mitandao hii. 
Kama umeshafanya njia hizo mbili lakini bado huwezi kujizuia kutembelea mitandao hii kila mara, basi angalia ni kwa namna gani unaweza kunufaika na itandao hii. Yaani angalia unawezaje kuitumia kujiingizia kipato.

Na habari njema sana kwako ni kwamba kila mtu, narudia tena KILA MTU anaweza kutengeneza kipato kupitia mtandao wa intaneti.

Kwa kuanza, angalia ni vitu gani unapenda sana kutembelea kwenye mitandao hii, ni vitu gani unapenda kufuatilia zaidi. Ukishajua vitu hivyo angalia ni kwa namna gani unaweza kuwasaidia wengine wanaohitaji taarifa zinazohusiana na vile unavyopenda kufuatilia. Na hapo unaweza kuanzisha ukurasa maalumu kwa ajili ya mambo hayo na hata kuwa na blog au tovuti.

Pia unaweza kutumia mitandao hii kuboresha kazi unayofanya au biashara yako. unaweza kutumia mitandao hii kupata wateja wa kile unachofanya au kutoa taarifa kwa wale wanaohusika na unachofanya. Pia unaweza kutumia mitandao hii kufanya tafiti zinazohusu kazi au biashara yako. zipo njia nyingi za kunufaika ni wewe kuchagua kipi kinakufaa.

Jumatatu, 18 Julai 2016

Mwaimbaji Shaa Aikacha MJ Records, Adai Hayupo Tena Katika Lebo Hiyo Inayomilikiwa na Master Jay


Malikia wa uswazi kama mwenyewe anavyopenda kujiita Shaa ameweka wazi zile tetesi zilizokuwa zimezagaa kwamba ameondoka Mj Record na kesema ni kweli hayupo chini ya lebo hiyo lakini haimaanishi kwa hafanyi kazi na studio za Mj .

Hata hivyo Shaa amesema ameanzisha kampuni yake inayoitwa SK ambayo ni matokeo ya kazi za sugua gaga,toba na nyingine ambazo zilirudisha gharama za Mj na kumuwezesha kufungua kampuni hake hiyo binafsi ambayo anatarajia kusajili wasanii hata wa tano ila kwa sasa yupo yeye peke yake.

Hata hivyo Shaa ameachia wimbo wake mpya unaoitwa Sawa kupitia kampuni yake hiyo ila unaambiwa Shaa hayupo taari kuyazungumzia mahusiano yake kama ailivyo mpenzi wake Master J ambaye akiulizwa na huwa anajibu lakini kwa Shaa nitofauti kabisaa

Wema Sepetu na Idris Sultam Wamwagana Rasmi

DAR ES SALAAM: Ubuyu wa motomoto wa mjini ni kwamba, zile mbwembwe zote za penzi la mastaa wawili Bongo, Wema Isaac Sepetu ‘Madam’ na Idris Sultan, zinadaiwa kufikia ukingoni na sasa imebaki stori kwani Wema, Idris wamwagana rasmi.

Wikienda limeng’atwa sikio kuwa, kitendo cha wawili hao ‘kushoo lavu’ kwenye ile Pati ya Black Tie iliyofanyika juzikati katika Ukumbi wa King Solomoni pale Namanga, Dar ilikuwa ni geresha tupu kwani walishamwagana kitambo.

Hata hivyo, kama utakumbuka au hukuipata ni kwamba iliwahi kuvujishwa kwenye mitandao ya kijamii kuwa Wema na Idris wamemwagana lakini baadaye zilivunjwa picha zikiwaonesha wakiwa wameshikana mikono na mahaba tele ili kuua soo.

wema-na-idriss-insta Sasa ubuyu ulionyooka kutoka kwa chanzo cha kuaminika ambacho ni mtu wa karibu wa mastaa hao unadai kwamba, kilichotokea kwenye pati hiyo zilikuwa ni mbwembe za kuzuga zilizotokana na huruma ya Idris.

Ilidaiwa kwamba, Idris alilazimika kufika kwenye sherehe hiyo kwa sababu ilishatangazwa kuwa atakuwa ni miongoni mwa ‘ma-hosti’ lakini ukweli ni kwamba mambo yalishaharibika.

wema na idris 2“Unajua watu wengi hawakujua kuwa Wema na Idris walishaachana kitambo na pale (King Solomoni) walikuwa wanafanya maigizo tu, japokuwa haijulikani moja kwa moja sababu ya kuachana kwao lakini Wema anadaiwa kuwa tatizo kwa Idris kutokana na kutokea kwa migogoro ya kila kukicha,” alitonya sosi huyo.

Hata hivyo, katika kuonesha kwamba kuna kitu kinaendelea, wana-ubuyu wetu walifuatilia akaunti zote za mastaa hao katika mitandao ya kijamii kuona kama mbwembwe zao zinaendelea na kubaini kuwa hawako sawa baada ya kusoma ujumbe wa Wema unaoonesha kumbembeleza Idris huku jamaa huyo akionesha wazi kuwa hakuna mapenzi bali ni drama tu.

Ili kuleta ushahidi, tunakukaribisha hapa kusoma nukuu zao mtandaoni;

MANENO YA WEMA
“Having you as a friend, a brother, a lover and of course a shoulder to cry on every time, i’m at my worst has been the best feeling ever… I wouldn’t want to lose this feeling over anything…
“I realized without u then i ain’t complete…. You have stood by me in good times and bad and even when i messed up so bad you would look me in the eyes and tell me, “Baby, its okay, we gona fix this”…
“Idris you have been one of a kind and losing u is the last thing i want on this earth… I will love you until forever, until death do us part we will be together…
“I will hold on to you till da last minute because together we will get there…. I love you with my life…. For I believe you are my true love, my baby and inshallah! The Man that my kids will call daddy…” alimalizia kuandika Wema akimlilia Idris.

IDRIS NAYE ALIANDIKA:
“Kumbuka kurekebisha kiatu kila hatua ya maisha unayopiga kisije kuchomoka ukakanyaga mwiba ukapunguza spidi.”

WEMA ASAKWA
Wikienda halikuishia hapo kwani lilimsaka Wema anayedaiwa kubwagwa, alipopigiwa simu hakupokea, akaandikiwa ujumbe mfupi wa sms ambao pia hakuujibu.
Pia alitumiwa ujumbe kwa njia ya WhatsApp lakini pia hakujibu.

 UBUYU WAKAMILIKA KWA IDRIS MWENYEWE
Wikienda liligeuza dira yake na kuielekeza kwa Idris ambaye alifunguka bila kuacha lolote.
Kwa mujibu wa Idris, yeye na Wema walishasahau kuwa waliwahi kuwa na uhusiano wa kimapenzi kwani kwa sasa kila mtu ana ‘biashara’ zake.

“Mimi nilikwenda kwenye ile pati kwa sababu ya kuwaonea huruma tu kwani ndiyo kwanza wameanzisha kampuni na mbaya zaidi walikuwa wakiniweka kwenye matangazo. Unadhani watu wangewachukuliaje? Sikutaka kuwaharibia shoo lakini mimi nilishaachana naye na nina biashara zangu nyingine,” alifunguka Idris.

Idris alienda mbali zaidi na kusema kuwa kwa sasa ana mwanamke mwingine anayempenda na siku si nyingi mambo yakikaa sawa, atamuanika.
“Mwenzenu nina kifaa kingine soon nitawafahamisha,” alisema Idris.

WEMA NA IDRIS
Awali Wema na Idris walificha uhusiano wao lakini baadaye waliamua kujiachia ambapo mlimbwende huyo alidai kushika ujauzito lakini kwa bahati mbaya ukachoropoka.

Source:Global Publishers

Auawa Kwa Kukatwa Kichwa..Kiwiliwili Chatelekezwa Bila Kichwa

Mtu mmoja amefariki dunia kwa kukatwa kichwa na kiwiliwili chake kutelekezwa kichakani katika Kijiji cha Rushwa, Kata ya Mushabago, Wilaya ya Muleba mkoani Kagera.

Mwenyekiti wa Kitongoji cha Buyango, Gasper Joseph amesema wamelazimika kuita wananchi ili kuutambua mwili wa marehemu.

Amesema licha ya kiwiliwili kutelekezwa kwenye eneo la kichaka, kichwa cha marehemu huyo wa kiume hakikuwapo kwenye eneo hilo jambo ambalo alilosema limeleta hofu kwa wananchi.

“Nimeita watu na walikusanyika, hata hivyo walishindwa kuubaini mwili huo kwa kuwa kichwa chake hakikuonekana. Mwenyekiti wa Kijiji cha Rushwa alitoa taarifa polisi kwa ajili ya hatua zaidi ili turuhusiwe kuzika,” amesema Joseph.

Staa wa Pakistan Auawa na Kaka yake Aliyechukia Picha Alizokuwa Akiweka Kwenye Mitandao ya Kijamii

Qandeel Baloch, aliyekuwa miongoni mwa mastaa wa mitandao ya kijamii nchini Pakistan, ameuawa na kaka yake katika mji wa Multan uliopo kwenye jimbo la Punjab. Alidai amemuua dada yake kwa heshima.

Polisi wamedai kuwa Baloch aliuawa na kaka yake kwenye nyumba ya familia yao baada ya kuchukizwa kwa muda mrefu na picha ambazo dada yake alikuwa akizipost mtandaoni.

Mwili wa mrembo huyo ukipelekwa kuzikwa

Baada ya kutekeleza mauaji hayo kaka yake alikimbia japo baadaye alikamatwa na polisi na kukiri kuhusika mbele ya waandishi wa habari.
Msichana huyo alikuwa akiweka picha za kawaida ambazo mastaa wengine duniani hupenda kuziweka kuonesha urembo wao.


Hata hivyo kwa maisha ya Pakistan na sheria zake, Baloch alionekana kuwa ‘controversial’ japo alipendwa sana.

Alikuwa na karibu wafuasi 750,000 kwenye mtandao wa Facebook ambako video zake zilikuwa maarufu na kuzalisha mijadala nchini humo.


Alijipatia umaarufu zaidi nchini humo baada ya kuahidi kuwa angevua nguo online kama timu ya Pakistan ingeshinda kwenye mchezo wa  cricket dhidi ya mahasimu wao India.

Baloch alitengeneza pia vichwa vya habari baada ya kupost selfie kwenye Instagram akiwa na Mufti Abdul Qavi, moja ya viongozi wa dini nchini humo na kupelekea kusimamishwa wadhifa huo.
Kaka yake alidai kuwa skendo zake ndizo zilimfanya achukue uamuzi wa kumuua.

Bongo5

Jumapili, 17 Julai 2016

Mtanzania Awekwa Bondi na kaka yake kisa Madawa ya kulevya huko India. Sambaza Habari hii iwafikie ndugu zak


Mtanzania amuweka mdogo wake Bondi kwaajili ya Madawa ya kulevya huko INDIA sasa wenye mzigo wamecharuka wanataka pesa zao hali sio nzuri kabisa kwa mdogo mtu Haya ndio maneno yalio sikika akiyasema Mdogo mtu kwenye Video hii.

“Nakaa Magomeni  Mtaa chem Chem na Idrisa kwa hiyo Mwambieni  Juma, Mama yangu anaitwa Rukia Daudi Baba yangu anaitwa Akida anakaa idrisa na Chem Chem mwambieni  Juma amekula Hela za watu mimi kaniweka Gelenta huku ( Bondi ) mama yangu anaitwa Rukia Daudi mama yake mama yake Juma anaitwa Mariamu Rauwa kwaiyo juma afanye arudishe hela za watu Juma anakaa Kunduchi”. kama unamfahamu huyo Juma mama yake mfikishie ujumbe huu..

Sambaza Habari hii imfikie JUMA na ndugu zake kokote walipo..


 Angalia Video hii Hapa.. 

VIDEO:WEMA AKIMBUSI OMY DIMPOZ

dinsta


Video wema sepetu K1ssing Omy Dimoz,Idris sultan will kill Omy Dimpoz after seeing this video of wema 


Millen Magese stuns on new Bik1ni Photos



From Millen's Body to some serious Lupron Body it must go down . Kudos to all women who goes through IVF treatments . The hormones are crazy phe
Do things that makes you happy